Skip to main content
Skip to main content

Wakazi 2,500 watibiwa magonjwa tofauti bila malipo Engwen, Nandi

  • | Citizen TV
    183 views
    Duration: 2:03
    Wakazi 2,500, wakiwemo wazee na vijana kutoka eneo la Engwen katika Kaunti ya Nandi, wamepata afueni baada ya kunufaika na kambi ya matibabu bila malipo na kampeni ya uhamasishaji dhidi ya utumiaji wa dawa za kulevya. Kambi hiyo ya matibabu, iliyoandaliwa na kundi la wasamaria wema pamoja na wanafunzi wa utabibu kati chuo kikuu cha Moi, iliwaleta pamoja wataalamu wa afya ambao walitoa huduma za kipekee, ushauri wa kitaalamu, na dawa kwa wagonjwa mbalimbali.