- 2,439 viewsDuration: 1:55Serikali imeanzisha uchunguzi kuhusu madai ya unyanyasaji dhidi ya wanawake wa Kenya unaodaiwa kutekelezwa na raia wa Urusi, kufuatia kusambazwa kwa video zilizosambaa mitandaoni. Katika taarifa, Wizara ya Jinsia imeagiza vyombo vya usalama kuchukua hatua za haraka kuchunguza suala hilo. Video hizo, ambazo zimezua hasira kubwa miongoni mwa wakenya, zilisambazwa sana mwishoni mwa wiki na kuchochea mdahalo, dhihaka na lawama mtandaoni.