Huku ikiwa imesalia siku moja tu kwa Waislamu kuanza mwezi mtukufu wa Ramadhani, hali ya ukame inaendelea kuwa mbaya katika maeneo ya Kaskazini Mashariki mwa nchi, ambapo wakazi wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula na maji, huku mifugo wengi wakiripotiwa kufa kutokana na ukosefu wa malisho na maji.
Katika juhudi za kupunguza makali ya hali hiyo, aliyekuwa Mbunge wa Wajir Kusini, Mohamud Sheikh Omar, ametoa msaada wa chakula kwa zaidi ya familia elfu thelathini zilizoathirika na ukame katika eneo La diif .Wakati huo huo, ameitaka serikali ya kitaifa na ile ya kaunti kuharakisha juhudi za kutoa msaada wa dharura kwa wakazi wa Kaskazini Mashariki, akisema hali ya ukame imeathiri pakubwa maisha ya wananchi na mifugo wao ambao ndio tegemeo kuu la uchumi eneo h