- 250 viewsDuration: 1:31Wawekezaji wengi wa reja reja wa humu nchini walisusia kuwekeza katika hisa za kampuni ya Kenya Pipeline wakipata asilimia 2.56 pekee ya hisa zilizouzwa. Hata hivyo waziri wa hazina ya kitaifa john mbadi anasema serikali imepata shilingi bilioni 106 kutoka uuzaji huo. Wengi wa wawekezaji wakiwa taasisi za humu nchini waliopata asilimia 41 ya hisa. Serikali ya kenya itasalia na asilimia 35 ya hisa.