- 1,479 viewsDuration: 32sMwakilishi wa Kike wa Kaunti ya Trans Nzoia Lilian Siyoi, ameitaka serikali kupitia Bunge kuangazia upya sheria zinazohusu mauaji, akisema kuwa washukiwa wa makosa hayo hawafai kupewa dhamana.Akizungumza katika eneo la Saboti, Siyoi ametoa kauli hiyo kutokana na kisa cha kusikitisha ambapo msichana mwenye umri wa miaka minane alinajisiwa na kuuawa kisha mwili wake kutupwa katika shamba la mahindi na mtu asiyejulikana wiki jana.