1,665 views
Duration: 3:12
Jinsi maandamano ya Gen Z yalivyo pindua serikali ya Nepal.
Kuna wanaosema kufungiwa kwa mitandao ya kijamii ndiyo kumesababisha mandamano hayo.
Lakini wanazuoni wabobezi wa masuala ya Nepal wanasema kufungwa kwa mitandao ya kijamii, kumekuwa ni cheche tu iliyolipua bomu lililokuwa likitokota kwa muda mrefu
Bomu lenyewe ni mchanganyiko wa matumizi mabaya ya serikali na vibaraka wake, rushwa, Uchumi kudorora na ukosefu mkubwa wa ajira miongoni mwa vijana
Kwa miaka mingi, Uchumi wa Nepal umekuwa ukishikiriwa na pesa zinazotumwa nyumbani na WanaNepal waliokwenda nje ya nchi kutafuta ajira
Kulingana na ripoti ya hivi karibu, ndani ya mwaka mmoja karibu WanaNepal Laki Nne na Nusu walikwenda nje ya nchi kutafuta ajira.
Lakini je, Kufungwa mitandao ya kijamii kumetoka wapi?
-
-
#bbcswahili #mitandaoyakijamii #nepal #rushwa #vijana