Msemaji wa Iraq asema shambulizi la Marekani 'ni mauaji dhahiri'
Iraq siku ya Alhamisi imeikosoa vikali shambulizi lililofanywa na droni ya Marekani ambalo jeshi lake lilisema limemuua kiongozi wa kikundi cha wanamgambo kinachoungwa mkono na Iran.
Msemaji wa Iraqi ameliita shambulizi hilo “ni mauaji dhahiri” ambayo yanaonyesha “kutothamini maisha ya raia au sheria za kimataifa.”
Yehia Rasool, msemaji wa waziri mkuu wa Iraqi, alisema kuwa ushirika unaongozwa na Marekani ambao umekuwa na operesheni nchini Iraq kukabiliana na kikundi cha Islamic State “mara kwa mara imekwenda kinyume na sababu na malengo ya uwepo wake katika eneo letu.”
“Mwelekeo huo unailazimisha serikali ya Iraqi kuchukua hatua kuliko wakati wowote mwengine kusitisha kazi ya ushirika huu, ambayo imekuwa ni sababu ya kutokuwepo utulivu na kutishia kuingiza Iraq katika wimbi la vita,” Rasool alisema katika taarifa yake.
Kamandi Kuu ya Marekani, ambayo inasimamia operesheni za kijeshi za Marekani katika Mashariki ya Kati, ilisema kuwa shambulizi la Jumanne lililomuua kamanda wa kikundi cha wanamgambo Kataib Hezbollah ambaye “alihusika moja kwa moja kupanga na kushiriki katika mashambulizi dhidi ya majeshi ya Marekani katika kanda hiyo.”
Maafisa wawili wa Marekani wamethibitishia VOA kuwa kamanda huyo alikuwa ni afisa wa operesheni Wisam Mohammad al-Saedi. Picha katika mitandao ya kijamii zilidai kuonyesha kitambulisho chake cha Iraqi ambacho kilichomolewa kutoka katika mwili wake.
VOA mapema iliripoti kuwa jeshi la Marekani lilikuwa limehusika katika shambulizi la anga dhidi ya lengo lenye umuhimu wa juu katika Mashariki ya Kati lakini ilikuwa haijamtambua al-Saedi kwa jina lake.
Kanda ya video iliyokuwa imesambazwa katika mitandao ya kijamii inaonyesha gari moja lililokuwa linawaka moto katika barabara kuu ya Baghdad.
Shambulizi la Marekani lilikuwa kulipiza kisasi mashambulizi takriban ya droni 170, roketi na makombora yaliyotekelezwa dhidi ya majeshi ya Marekani huko Mashariki ya Kati tangu katikati ya Oktoba, mojawapo liliuwa wanajeshi watatu wa Marekani na kujeruhi wengine zaidi ya darzeni kaskazini ya Jordan wiki iliyopita.
Ripoti ya mwandishi wa VOA Chris Hannas
#Haifa #waelaldahdouh #hamzaaldahdouh #shirikalamwezimwekundu
#Rafah #Netanyahu #Misri #Hamas #Gaza #Palestina #IDF #GalMeirEizenkot #iran #iraq
13 Aug 2025
- The president had previously hosted thousands of youths at State House.
13 Aug 2025
- China expects to import 2,000 tonnes of macadamia by the end of the year.
13 Aug 2025
- The MP has shown interest in running for governor of Nairobi.
13 Aug 2025
- President William Ruto on Wednesday assented to the County Allocation of Revenue Bill, 2025, and the County Public Finance Laws (Amendment) Bill, 2023.
13 Aug 2025
- The ruling follows a petition filed by four individuals, among them Nakuru-based surgeon Dr. Benjamin Gikenyi, challenging the legality of the committee appointed to audit pending NHIF claims.
13 Aug 2025
- The president had previously hosted thousands of youths at State House.
13 Aug 2025
- China expects to import 2,000 tonnes of macadamia by the end of the year.
13 Aug 2025
- "Tusiharibu game tumestruggle sana kuijenga.”
13 Aug 2025
- Senior officials from the British Army Training Unit Kenya (BATUK) failed to appear in Parliament on Tuesday to answer questions about the atrocities their soldiers have committed in the country.
13 Aug 2025
- African officials and experts have warned that the unpredictability of U.S. trade policy fuels uncertainty for the continent's development.
13 Aug 2025
- Staying in touch with friends and family accounts for 60.2% of usage.
13 Aug 2025
- For those with visual impairments, female ownership is slightly higher at 70.8% compared to males at 66.1%.
13 Aug 2025
- Widow says she warned her late husband against following suspected cult leader's teachings.