- 692 viewsDuration: 2:36Zaidi ya familia 300 kutoka kijiji cha Mkocheni kaunti ya Taita Taveta zimeachawa bila makao baada ya nyumba zao kubomolewa kufuatia utata wa ardhi. Familia hizo zimeachwa njiapanda baada ya ilani waliyopewa kuwataka kuhama ardhi hiyo ya ekari elfu moja kufikia leo. Ubomoaji huu umefanywa huku wanakijiji hao wakiwa na ilani ya mahakama kuzuia hatua hiyo