- 342 viewsDuration: 1:45Walimu wa shule za sekondari msingi eneo la Kipini kaunti ya Tana River wanaitaka serikali kuwapa walimu wa JSS uhuru wa kujisimamia. Kulingana na walimu hao, kuunganishwa kwao na walimu wa shule za msingi kunawapa changamoto kutekeleza mfumo wa elimu wa CBC. Walimu hao pia wanaitaka tume ya uajiri wa walimu TSC kuajiri walimu zaidi wa JSS ili kutatua changamoto ya walimu kufunza masomo ambayo hawajahitimu.