Waokoaji: 'Jeshi la Israeli laacha miili mingi mjini Gaza City'
Waokoaji walisema majeshi ya Israeli yameacha darzeni za miili walipoondoka maeneo mbalimbali ya Gaza City usiku baada ya mashambulizi makali yaliyodumu kwa wiki nzima ambayo yalikabiliwa na wapiganaji wa Hamas wakikabiliana nao. Waokoaji walisema wameikusanya kiasi ya miili 60 hadi sasa.,
Jeshi hilo lilitoa kanda ya video Jumatano (Julai 10) ikionyesha kile walichosema ni majeshi ya ardhini yakifanya operesheni Gaza wakati mashauriano ya kusitisha mapigano katika vita vilivyodumu kwa miezi tisa yamepangwa kuanza tena.
Jeshi la Israeli lilisema katika taarifa yake kuwa majeshi yake yalikuwa yanaendelea na operesheni huko Gaza City dhidi ya wanamgambo wa Hamas na washirika wao Islamic Jihad, ambao walisema walikuwa wanafanya mashambulizi kutoka katika kituo cha UNRWA, wakikitumia kama ni ngome yao ya kufanya mashambulizi.
Kulingana na jeshi la Israeli walikuwa wamefanyia operesheni zao katikati mwa Gaza na Shejaiya.
Shirika la habari la Reuters halikuweza kuthibitisha eneo linaloonyeshwa katika kanda ya video. Reuters imeshindwa kupata uthibitisho huru wa tarehe ambayo video hiyo ilichukuliwa.
Vita hiyo ilianza Oktoba 7 wakati wapiganaji kutoka Palestina wa kikundi cha wanamgambo wa Hamas walipovamia mpakani na kushambulia jamii mbalimbali huko Israel, ikiuwa watu 1,200 na kuwateka watu 250, kulingana na idadi iliyotolewa na Israeli.
Shambulizi la Israeli huko Gaza kulipiza kisasi lilianza siku hiyo hiyo kwa kushambulia kwa mabomu na limeendelea kwa miezi tisa pamoja na uvamizi wa ardhini ambapo mamlaka za afya Palestina zinasema imeuwa zaidi ya watu 38,000 na kujeruhi zaidi ya watu 80,000.
Idadi kubwa ya waliojeruhiwa kutokana na vita hivyo imeongeza magonjwa kusambaa na utapiamlo kati ya wakazi asilimia 90 wa Gaza ambapo Umoja wa Mataifa unasema wamekoseshwa makazi, na kuweka shinikizo kubwa kwa mifumo ya afya katika eneo hilo finyu. - Reuters
#Rafah #Netanyahu #Misri #Hamas #Gaza #Palestina #IDF #GalMeirEizenkot #mauaji #jeshi #israel #voa #voaswahili #mwandishi #aljazeera #maghazi #wahouthi #marekani #uingereza #shambulizi #dhamar #yemen #hospitali #nasserhospital
9 May 2025
- Lucrative job offers had been posted about employment in South Korea.
9 May 2025
- He was elected on Thursday, May 8, to replace Pope Francis, who passed away in April.
9 May 2025
- Erastus Ethekon was nominated by President William Ruto upon the recommendation of the IEBC selection panel.
9 May 2025
- The nine family members who perished in a suspected arson attack in Ugunja, Migori County will be laid to rest today (Friday).
9 May 2025
- Pope Leo XIV will celebrate mass Friday, the day after becoming the first US head of the Catholic Church, with the world watching for signs of what kind of pope he will be.
9 May 2025
- Residents of Nyangores in Chepalungu Constituency, Bomet County, are asking the county government to urgently repair a bridge that continues to endanger the lives of students and pupils.
9 May 2025
- Ukraine's parliament voted Thursday to ratify a long-awaited minerals deal with the United States, an agreement Kyiv hopes will pave the way for future military support from Washington.
9 May 2025
- Rwanda's economy is forecast to grow at a slower pace this year than in 2024, while government spending for the 2025/26 fiscal year is expected to rise by about a fifth, Finance Minister Yusuf Murangwa said on Thursday.
9 May 2025
- Bill Gates pledged on Thursday to give away Ksh.25.8 trillion via his charitable foundation by 2045 and lashed out at Elon Musk, accusing the world's richest man of "killing the world's poorest children" through huge cuts to the U.S. foreign aid budget.
9 May 2025
- Lucrative job offers had been posted about employment in South Korea.
9 May 2025
- Kenya’s Ambassador to Belgium, Prof. Bitange Ndemo, has declined his appointment as the new Vice Chancellor of the University of Nairobi (UoN), citing procedural irregularities.
9 May 2025
- Former US president Joe Biden said Thursday he was not surprised Kamala Harris lost the 2024 election to Donald Trump and blamed her defeat on Republicans taking the "sexist route."
9 May 2025
- Safaricom was the first private telecom operator to break the state-owned monopoly of Ethio Telecom.