Afisa wa polisi James Mukhwana apasua mbarika kuhusu kifo cha Albert Ojwang

  • | Citizen TV
    69,615 views

    Afisa wa polisi James Mukhwana, ambaye anazuiliwa kuhusiana na mauaji ya mwanablogu Albert Ojwang’, amepasua mbarika akidai kupewa maelezo ya kumtia adabu. Mukwana akisema mkuu wa kituo cha Central Samson Taalam alimpa maelekezo haya ambayo yaliripotiwa kutoka kwa naibu inspekta wa polisi aliyejiondoa Eliud Lagat. Kwenye taarifa yake kwa IPOA, Mukhwana amekiri kusema uongo kwenye taarifa ya awali.