Angola yasema itajaribu kusimamia mazungumzo kati ya DRC na M23
Angola imesema siku ya Jumanne itajaribu kusimamia mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda katika siku zijazo.
Haikufahamika iwapo serikali ya Congo, ambayo ilikataa mara nyingi kufanya mazungumzo na M23, itashiriki katika mazungumzo hayo.
Msemaji wa ofisi ya rais wa Congo aliiambia Reuters mamlaka hiyo imezingatia hatua hiyo, wakati naibu msemaji wa M23 alisema ulikuwa “ni ushindi wa hoja” na kuthibitisha ushiriki wa kikundi hicho katika mazungumzo hayo.
Rais wa DRC Felix Tshisekedi alifanya ziara ya kikazi mjini Luanda na alikutana na mwenzie Joao Lourenco, ofisi ya rais wa Angola ilisema katika taarifa kwenye Facebook.
“Angola kama mpatanishi katika mzozo wa mashariki mwa Congo, itaanzisha mawasiliano na M23, ili wajumbe kutoka Congo na M23 wafanye mazungumzo ya moja kwa moja mjini Luanda katika siku zijazo,” ofisi ya rais iliongeza.
Nchi hiyo iliyoko Kusini mwa Afrika imekuwa ikijaribu kusimamia kufikiwa kwa sitisho la mapigano na kupunguza mivutano kati ya Congo na jirani yake Rwanda, ambayo imekuwa ikishutumiwa kuwasaidia kikundi cha waasi wa Kitutsi.
Rwanda imekanusha kuwapa msaada wa silaha na wanajeshi waasi wa M23, na imesema majeshi yake yanajihami dhidi ya jeshi la Congo na wanamgambo wenye chuki na Kigali.
Waasi wa M23 wamekamata miji mikubwa miwili iliyoko mashariki mwa Congo tangu Januari katika mvutano wa mgogoro wa muda mrefu ambao kiini chake ulisambaa Congo kutokana na mauaji ya halaiki ya Rwanda yam waka 1994 na juhudi ya kutaka kudhibiti eneo kubwa lenye madini nchini Congo.
#angola #waasi #m23 #congo #felixtshisekedi #JoaoLourenco #rwanda
20 Mar 2025
- The accident occurred in Kakamega and involved several wagon with goods destined for Uganda.
20 Mar 2025
- The nomination comes nine months after she lost her Cabinet position.
20 Mar 2025
- Rumours have been swirling for some time now that changes to PSs were imminent.
20 Mar 2025
- Former CS Susan Nakhumicha Wafula can now breathe a sigh of relief after President William Ruto seemingly plucked her from perceived political obscurity, bringing her back into the fold with the nomination to a new role.
20 Mar 2025
- President William Ruto has instituted changes in government to accelerate the implementation of the Bottom-Up Economic Transformation Agenda (BETA).
20 Mar 2025
- President William Ruto has instituted changes in government to accelerate the implementation of the Bottom-Up Economic Transformation Agenda (BETA).
20 Mar 2025
- A deadly outbreak of Kala-azar, a parasitic disease caused by the Leishmania parasite, has hit Wajir County, leaving 18 dead and infecting more than 500 people in the last 3 months.
20 Mar 2025
- Journalists covering a Thursday meeting convened to challenge business rates and levies imposed by Kiambu County were attacked and their equipment destroyed and stolen by goons, allegedly hired by MCAs believed to be supporters of Governor Kimani…
20 Mar 2025
- Armed men shot and killed four people at a taxi rank in central Johannesburg on Thursday, South African police said, reporting a similar shooting near the city the day before that killed three others.
20 Mar 2025
- A dossier related to the 1963 assassination of U.S. President John F. Kennedy, released by President Donald Trump's administration, has revealed how Kenya provided an operational base for the Central Intelligence Agency (CIA).
20 Mar 2025
- The judge also noted that Prof. Kisiang'ani had exceeded his authority, stating that such a policy decision could only be legally made by the Treasury Cabinet Secretary.
20 Mar 2025
- Peter Tum also picked as envoy to Kinshasa.
20 Mar 2025
- They say the governor has been absent from key county affairs, yet she should be back from maternity leave.