BBC Africa Eye: 'Nina ugonjwa ambao siwezi kutofautisha kitu halisi na kisicho halisi'

  • | BBC Swahili
    1,064 views
    Hii ni simulizi ya kina ya kuishi na ugonjwa unaofahamika kama 'Bipolar' nchini Kenya, ambapo suala la afya ya akili mara nyingi linaonekana ni mwiko na lisilopewa uzito wake kwenye jamii. Noella Luka alikuwa na ndoto kubwa ya kuwa mtayarishaji filamu akienda kusomea fani hiyo nchini Marekani, lakini mambo yalibadilika ghafla baada ya kupata tatizo la afya ya akili na kubadili kila kitu katika maisha yake. Fuatilia makala haya ya BBC Africa Eye. Picha: Noella Luka