- 313 viewsDaktari wa Kipalestina Khaled al-Saedni anafanya kazi katika kitengo cha watoto cha hospitali ya Al-Aqsa Martyrs huko Gaza City. Daktari huyu, ambaye amefanya kazi katika hospitali hii kwa zaidi ya miaka 23, alipoteza mguu wake mwaka jana baada ya kujeruhiwa. Anasema alijeruhiwa na bomu katika kambi ya wakimbizi ya Al-Bureij katika miezi ya kwanza ya vita vya Gaza. Kutokana na matatizo yaliyotokana na maradhi ya kisukari, daktari huyu mwenye umri wa miaka 50 anasema, mguu wake ulikatwa. Lakini licha ya kutegemea kifaa cha kutembelea, daktari huyu wa watoto alisema amerejea kufanya kazi kuwahudumia watoto “katika fursa ya kwanza” aliyopata baada ya miezi kadhaa ya kufanyiwa upasuaji na kupata matibabu. “Nimepoteza mguu, namshukuru Mungu. Kuna watu familia zao nzima wamekufa shahidi – wake, watoto, wazazi na ndugu zao,” Saedni alisema, ana matumaini vita vya Gaza vitamalizika haraka. Israel ilianza mashambulizi ya angani na ardhini dhidi ya Gaza baada ya wapiganaji walioongozwa na Hamas kushambulia jamii za Waisraeli Oktoba 2023, na kuua watu 1,200 na kuwachukua mateka 250 kurejea nao Gaza, kulingana na hesabu za Isreali. Kampeni ya kivita ya Israeli tangu wakati huo imewauwa zaidi ya Wapalestina 46,500 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 100,000, kulingana na wizara ya afya ya Gaza. Kampeni hiyo imewakosesha makazi watu milioni 2.3 na kuharibu eneo lote finyu la pwani. #ukandawagaza #daktari #khaledalsaedni #israel #mabomu #hamas #mateka #voa #voaswahili #kilema
Daktari
- - Duniani Leo ››
- 17 Jun 2025 - Someone within government circles labelled him a prime suspect at a meeting of top officials.
- 17 Jun 2025 - According to United Nations Population Fund, persons with disabilities make up 2.2 per cent of the population — about 900,000 people.
- 17 Jun 2025 - The plastic waste menace birthed the idea to produce fuel from plastics, he says
- 17 Jun 2025 - The actual figure may be higher, as some counties did not disclose their borrowing
- 17 Jun 2025 - Imlu says underlying bad blood where NPS officers have reportedly refused to cooperate could stall investigations.
- 17 Jun 2025 - The appellate court agreed that this crucial detail had been ignored.
- 17 Jun 2025 - Thousands of civil servants serving in positions of directors and above have been left in utter shock after the government set standards that require them to have Master’s Degrees. The Public Service Commission (PSC) has sent shockwaves through the…
- 17 Jun 2025 - Last week’s high-level meeting in Changsha between China’s top diplomat Wang Yi and representatives from 53 African countries sent a powerful and optimistic message: China is moving with clarity and purpose to implement the 10-point action plan unveiled…
- 17 Jun 2025 - Christine Riaro and her all-star team of Tabitha Ojwang, Joyce Osike and Griffins Owino extended their dominance a the 12th leg of the KCB East Africa Golf Tour at Nyanza Golf Club, sealing a third consecutive victory at the Nyanza leg with a combined…
- 17 Jun 2025 - A 35-year-old fisherman died in a police holding cell at Kipasi Police Post in Suba North Constituency, Homa Bay County, raising fresh concerns over the security of individuals being detained in police custody. The incident comes after the controversial…