- 1,185 viewsDuration: 3:02Familia ya mtu mmoja kati ya wawili waliofariki baada ya vurugu zilizoshuhudiwa jijini Kisumu Jumapili imeomba serikali kudhibiti visa vya uhuni vinavyosababisha maafa. Dickson Odiwuor, mwenye umri wa miaka 31, alifariki baada ya kudungwa kisu wakati vurugu zilipozuka kufuatia makabiliano kati ya makundi mawili ya wahuni. Wakati huo huo, viongozi wa Kisumu wamekashifu machafuko hayo na kuzitaka asasi za usalama kuwajibika na kuchukua hatua madhubuti kukabiliana na magenge ya wahuni.