Gavana Wa Kisumu atangaza kuwafidia baadhi ya waathiriwa wa ubomoaji

  • | Citizen TV
    299 views

    Gavana wa Kisumu Anyang Nyongo amesema kuwa serikali ya kaunti itafidia baadhi ya waathiriwa waliyopoteza mali yao kutokana na ubomoaji jijini humo. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kanuni za maendeleo za jiji la Kisumu, gavana Nyongo alisema kuwa serikali yake itabuni sheria zitakazotoa mfumo wa fidia kwa waathiriwa wa ubomoaji. Haya yanajiri wakati ambapo mashirika mbalimbali yamewasilisha malalamishi kortini dhidi ya serikali ya kaunti kufuatia ubomoaji katika muda wa miaka mitatu iliyopita. Baadhi ya miradi itakayotekelezwa katika kanuni hizo ni pamoja na ujenzi wa majumba ya kisasa na barabara.