Idadi ya waliofariki kwenye ajali iliyohusisha basi la Chuo Kikuu cha Pwani na matatu yafikia 17

  • | Citizen TV
    1,038 views

    idadi ya waliofariki kwenye ajali iliyohusisha basi la chuo kikuu cha Pwani na matatu katika eneo la Naivasha imeongezeka na kufikia watu 17. Hii ni baada ya watu wengine watatu kufariki kutokana na majeraha waliyopata. Wanafunzi kumi na mfanyikazi mmoja wa chuo kikuu cha Pwani walifariki kufuatia ajali hiyo iliyotokea katika barabara ya nairobi kuelekea nakuru.manusura wanasema waliagizwa kufunga mikanda ya usalama muda mfupi kabla ya basi hilo kugonga matatu na kuanguka kwenye mtaro. waziri wa afya wa Nakuru Jackline Osore amesema watu 76 wametibiwa katika hoaspitali ya kaunti ya Naivasha huku waliofariki wakikata roho kwenye eneo la mkasa au wakitibiwa. watu 12 wamesafirishwa hadi katika hospitali ya Kenyatta na hospitali ya mkoa ya Nakuru kwa matibabu maalum. Basi hilo lilikuwa na wanafunzi 62.