Wakati taifa linapojiandaa kuadhimisha sikukuu ya Utamaduni, wizara ya biashara, viwanda na uwekezaji imezindua maonesho ya sanaa kwenye afisi zake jijini Nairobi kwa nia ya kuwajumuisha wasanii wa humu nchini kwenye mpango mpana wa kitaifa wa biashara. Katibu katika wizara ya biashara Regina Ombam amesema mpango huo unapiga jeki juhudi za serikali za kupanua uchumi kupitia ukuzaji wa mahuruji ya bidhaa za kitamaduni na ujasiriamali bunifu kama vitega uchumi vipya na mbinu za kubuni nafasi za ajira.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKN
Follow us on Twitter: https://twitter.com/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1tv
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#KBCchannel1 #Kenya #News