Katibu katika wizara ya usalama wa taifa Dkt. Raymond Omollo, amethibitisha kujitolea kwa Rais William Ruto kuongeza ufadhili katika sekta ya elimu. Akizungumza eneo bunge la Nyatike, kaunti ya Migori katika hafla tofauti mbali mbali , Dkt Omollo alisema takriban asilimia 30 ya bajeti ya kitaifa imetengewa elimu ili kurahisisha uajiri wa walimu na ujenzi wa madarasa kote nchini. Alibainisha kuwa serikali ina mpango wa kuajiri walimu laki-1 ili kukabiliana na upungufu uliopo, pamoja na ujenzi wa madarasa zaidi ya 23,000 na maabara 11,000 kote nchini
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive