- 111 viewsTimu ya Kenya Police Bullets wametawazwa mabingwa wa Ligi Kuu kwa wanawake nchini kwa mwaka wa tatu mfululizo. Bullets wamemaliza msimu wao kwa ushindi wa bao moja bila dhidi ya Madira Soccer Assassins na kukamilisha msimu kwa alama 52. Wakati huo huo, timu za Kisumu All Starlets, Kisped Queens pamoja na Gideon Starlets zimeshushwa daraja. Sasa Bullets watajiandaa kwa michuano ya CECAFA kusaka tiketi ya Klabu Bingwa Afrika kwa wanawake.