- 110 viewsDuration: 3:28Wakulima wa mhogo eneo la pwani wamekuwa wakihangaishwa na ugonjwa wa mchirizi kahawia pamoja na wadudu waharibifu. Ni jambo ambalo limekuwa likiwasababishia hasara kubwa na kuwakosesha mapato. Katika Kaunti ya Kilifi, mashamba ya majaribio ya mhogo ulioboreshwa vinasaba yanazidi kuvutia msisimko mkubwa, huku wakulima wakifuatilia kwa karibu mafanikio yake na kutathmini uwezo wa kuwaongezea mavuno na mapato. Denis Otieno anaangazia kilimo cha mihogo ya GM kwenye makala ya Kilimo biashara.