Kitengo cha dijitali cha RMS chazoa tuzo ya uvumbuzi ya MSK

  • | Citizen TV
    341 views

    Kitengo cha dijitali cha kampuni ya Royal Media Services kiliibuka bingwa kwenye tuzo za shirika la masoko -MSK- za mwaka huu, baada ya kujizolea tuzo ya uvumbuzi kwenye sekta ya habari. Hii ni mara ya pili kwa kitengo cha dijitali cha RMS kutuzwa, mwaka moja tu baada ya kuzinduliwa oktoba mwaka jana. Katika hafla iliyoandaliwa na Msk gala na ambayo iliaandamana na maadhimisho ya miaka 60 ya shirika hilo. Miamba wa mauzo pia walitambuliwa na kuzawadiwa kwenye hafla hiyo. Wengine waliotunikiwa walikuwa ni pamoja na kampuni za Kenya Wine Agencies Ltd, EABL, Coca Cola, GA Insurance na SCANAD miongoni mwa mengine