- 246 viewsDuration: 1:43Maafisa tabibu katika kaunti ya Bungoma wameapa kutorejea kazini hadi matakwa yao yatimizwe. Wahudumu hao wa afya wanataka mkataba wa maelewano kati yao na serikali ya kaunti ya Bungoma utekelezwe na ajira ya kudumu. Wakizungumza baada ya kuandaa maandamano ya amani, matabibu wanahoji kuwa serikali ya kaunti haijakuwa ikitilia maanani malalamishi yao wakisema hawatakubali kurejea kazini hadi wasikizwe.