- 12,006 viewsDuration: 3:04Hakusoma wala kutimiza ndoto yake ya kuwa mhandisi, ila mama mmoja kutoka kaunti ya Samburu Jecinta Lelukumani amesema ana imani yeye ni mhandisi wa kuzaliwa. Mama huyu wa watoto sita akisema ari yake ya kuwa mhandisi bila elimu baada ya kuozwa mapema kulimsukuma kuanza kujijengea mwenyewe manyatta ya ghorofa katika kijiji kidogo cha Baawa huko Samburu.