- 320 viewsDuration: 2:45Mashirika ya kijamii na watetezi wa haki za binadamu wanaishutumu serikali kwa madai ya kutumia polisi na vitisho dhidi ya wakosoaji wake. Makundi hayo yanadai kuwa maafisa wa mashirika ya kutetea haki za binadamu wanaishi kwa hofu baada ya kudaiwa kuandamwa na watu wasiojulikana na kuvamiwa kwa afisi zao na watu wanaodaiwa kuwa maafisa wa polisi. Sasa yanamtaka Inspekta Jenerali wa Polisi, Douglas Kanja, kuchunguza madai hayo.