- 3,022 viewsDuration: 1:38Maafisa wawili wa polisi wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji ya Shukri Adan Ibrahim katika mtaa wa Mukuru kwa Njenga baada ya mkurugenzi wa mashtaka kupendekeza washtakiwe baada ya IPOA kuwapata na hatia. Hata hivyo, hawakusomewa mashtaka baada ya wakili wa IPOA, Kevin Lusweti, kuieleza mahakama kuwa jaji anayeshughulikia kesi hiyo hakuwepo. hakimu Caroline Nyaguthii aliagiza suala hilo lisikizwe kwa njia ya mtandao ili kuruhusu uchunguzi kuendelea.Sajenti Godwin Mjomba na konstaboPatrick Mutunga Titus wanatarajiw akufikishwa mbele ya jaji Martin Muya kujibu mashtaka ya mauaji. Marehemu Shukri alipigwa risasi kichwani na kufariki. Familia yake imeitaka mahakama kuharakisha kesi hiyo.