- 449 viewsDuration: 2:56Wahadhiri na wafanyakazi wa vyuo vikuu wameapa kutorejea kazini huku mgomo wao ukiingia wiki ya tatu. Wakuu wa vyama vya UASU na KUSU wakisema ni lazima walipwe shilingi bilioni 7.9 zilizoafikiwa kwenye makubaliano ya mwaka 2017–2021. Waziri wa elimu, julius migos ogamba hata hivyo anasema serikali haikubaliani na kiwango hicho na itaelekea mahakamani jumatatu ijayo. Haya yanajiri huku masomo ya maelfu ya wanafunzi yakisalia njia panda