Mkanganyiko kuhusu kusitishwa kwa mgomo wa walimu wa sekondari msingi washamiri

  • | Citizen TV
    571 views

    Mkanganyiko unaendelea kushuhudiwa katika shule za sekondari msingi zinazomilikiwa na serikali baada ya muungano wa walimu wa sekondari (KUPPET) na baadhi ya viongozi wa JSS kutia saini mkataba wa kurejea kazini baada ya kile walikitaja kama makubaliano na mwajiri wa walimu tsc. Makubaliano hayo yakikanushwa na upande moja wa walimu hao wa JSS ambao wanasema hawakuhusishwa. Awali walimu hao amabo walikutana na muungano wa KUPPET walisitisha mgomo huku wenzao wakisisitiza kuwa mgomo utaendelea hadi pale wote watapata barua za kuajiriwa.