- 277 viewsDuration: 1:55Ni afueni kwa wenyeji wa Golbati na Ngao kaunti ya Tana River baada ya kukamilika na kuzinduliwa kwa mradi wa maji eneo hilo. Mradi huo uliyogharimu zaidi ya shilingi laki moja utafaidi familia elfu tisa ambapo maji pia yatasambazwa kwa miji ya Tarasaa na Oda eneo bunge la Garsen. Aidha mradi huu utapunguza visa vya vya watu na mifugo kuliwa na mamba kwenye mto Tana wanapoenda mtoni kutafuta maji. kadhalika utachangia pakubwa kwenye kilimo cha unyunyiziaji maji shambani.