Zaidi ya vijana 8,000 kutoka kaunti za Kisumu, Siaya na Homa Bay watapokea zaidi ya shiliüngi milioni 200 kutoka kwa serikali chini ya mpango wa Nyota. Akizungumza katika kaunti ya Kisumu Rais William Ruto alitangaza kuwa zaidi ya vijana laki 6 watapokea mafunzo kuhusu jinsi ya kunufaika na zabuni za serikali. Haya yanajiri huku utafiti uliofanywa na Shirika Ła Infotrak ukionyesha kwamba licha ya asilimia 78% ya wakenya kuwa na ufahamu kuhusu mpango wa Nyota, ni asilimia 36% pekee ambao wamenufaika.