Mvutano kati ya wakaazi waliofurushwa mtaani Woodley na kaunti ya Nairobi waendelea

  • | Citizen TV
    152 views

    Wakaazi waliofurushwa mtaa wa Woodley wameandamana leo wakiendelea kulalamikia kufurushwa kinyume na sheria. Kulingana nao, wahuni wanaotumwa kuwavuruga wamekuwa wakiwatishia kwa mtutu wa bunduki huku wakidai kuwa na hati miliki pamoja na amri ya mahakama kuhalalisha kuwepo kwao katika nyumba hizo. Amri ambayo imetupiliwa mbali na serikali ya kaunti ya nairobi. Sasa wanamtaka seneta wa nairobi edwin sifuna na serikali kuu kuingilia kati.