- 858 viewsPolisi katika eneo la Kajiado West wanawatafuta washukiwa zaidi ya 20 ambao walitoroka baada ya kufumaniwa na wanakijii wakichinja Punda 34 Kichakani jana usiku. Washukiwa waliochinja punda hao katika eneo la Ereteti wanaaminika kuwa katika mipango ya kusafirisha na kuuza nyama hiyo hapa Nairobi.