- 3,426 viewsDuration: 1:55Rais William Ruto ametia saini mswada wa miundomsingi ya kitaifa, itakayotoa mwongozo wa kufadhili miradi mikuu ya serikali kama vile reli, barabara kuu na kawi, ili kubadilisha taifa la kenya kufikia viwango vya mataifa yaliyoendelea zaidi. Akizungumza baada ya kutia saini sheria hiyo mpya, rais William Ruto amesema mradi wa kwanza utakaofadhiliwa na mpango huo ni uboreshaji na ujenzi wa uwanja wa ndege wa JKIA.