- 509 viewsDuration: 3:15Bunge la Seneti sasa linasema mgogoro uliokuwa unaendelea baina ya maseneta na Baraza la Magavana kuhusu uwajibikaji umetatuliwa. Kiongozi wa wengi katika bunge la Seneti Aaron Cheruiyot akiwaambia kikao cha bunge kwamba magavana walikubali kuondoa makataa yao kwa seneti. Maseneta hao walikubali kuendelea na mjadala wa mswada wa nyongeza ya mgao wa fedha kwa kaunti, huku kamati ya bajeti ya seneti ikipendekeza magavana kupewa shilingi bilioni 454 katika mwaka ujao wa kifedha.