- 6,965 viewsDuration: 1:41Wafanyabiashara wa Uhuru market wanakadiria hasara kubwa baada ya maduka yao kubomolewa mapema leo, huku wengi wakiiomba serikali kuwasaidia na kuwapatia maeneo mbadala ya kufanyia biashara. Serikali ya kaunti ya Nairobi ilikuwa imetoa notisi ya saa 72 kwa wafanyabiashara hao kuhama kutoka eneo hilo, ili kutenga nafasi ya kujenga soko jipya. Ubomoaji huo uliofanywa kwa kutumia matingatinga na mashine za kuchimba uliwaacha wafanyabiashara na muda mchache sana wa kuokoa mali yao