AFYA KWA WOTE
Naibu rais Profesa Kithure Kindiki amesema serikali inaendelea kuwalipia wakenya wasiojiweza milioni 2.2 bima ya afya ya jamii kama hatua inayonuiwa kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora ya afya kwa kila mmoja. Kindiki anatoa wito kwa wakenya kuendelea kujisajili katika halmashauri ya afya ya jamii (SHA), akisema serikali inalenga kuwasajili wakenya milioni 55 chini ya halmashauri ya afya ya jamii kufikia mwaka 2027. Wakati uo huo, spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang’ula anatoa wito wa umoja kwa jamii ya Waluhya pamoja na kujisajili kwa idadi kubwa eneo la magharibi ya nchi kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive