Serikali yazindua mbinu mpya ya kukausha mboga kwa kutumia miale ya jua.

  • | K24 Video
    99 views

    Wakulima katika maeneo kame nchini wamepata afueni baada ya serikali kuzindua mbinu mpya ya kukausha mboga kwa kutumia miale ya jua. Kupitia shirika la utafiti wa kilimo na mifugo nchini KALRO, teknolojia hiyo mpya inalenga kuhifadhi mboga na mazao mengine kwa muda mrefu bila kuharibika. Mbinu hiyo mpya inalenga kupunguza hasara wakulima wanayopata wakati wa mavuno, kuongeza mapato yao na kuhakikisha usambazaji endelevu wa mboga hata wakati wa kiangazi.