- 2,614 viewsDuration: 2:52Wizara ya Afya imetoa rasmi orodha ya huduma 36 za matibabu maalum ambazo zitakazolipiwa na mfuko wa Bima ya Afya ya kijamii, SHA. Waziri wa Afya Aden Duale, amesema kuwa hatua hiyo inalenga kuwawezesha wakenya kupata matibabu ya maradhi ambayo hayawezi kutibiwa humu nchini, nje ya nchi. Hatua hiyo pia inalenga kuwapunguzia mzigo wa kifedha wagonjwa. Lakini kama anavyoripoti emily chebet, japo ni afueni, bado wagonjwa wanalalamika kuwa fedha zinazolipwa na sha hazitoshi.