- 257 viewsDuration: 1:39Tume ya kuajiri waalimu TSC imeasema inashirikiana na asasi zengine za serikali kuhakikisha usalama wa waalimu walio katika maeneo yenye hatari kama maeneo ya kaskazini mwa nchi na maeneo mengine. Mwenyekiti wa tume hiyo Jamleck Muturi akizungumza na wanahabari katika shule ya kitaifa ya wavulana ya Makueni baada ya kuanzisha zoezi la kusajili waalimu watakao jaza nafasi zilizoachwa wazi baada ya walimu kuondoka amesema tayari serikali imetuma maafisa huko Garisa kuzungumza na waalimu kuhusiana na shambulizi la kigaidi lilitokea juzi na kumuuwa mwalimu. Jamleck Muturi anasema zoezi hilo linalenga kuhakikisha hakuna shule inakumbwa na changamoto ya waalimu baada ya walimu kuondoka kwani watakaoajiriwa watajaza nafasi za shule zilezile zilioachwa wazi.