- 192 viewsDuration: 1:39Tume ya ardhi nchini NLC imeendelea kukusanya taarifa kuhusu migogoro ya ardhi na dhuluma za kihistoria katika kaunti mbalimbali nchini. Kamishina wa Tume hiyo Tiyah Galgalo amesema jumla ya kesi 1,864 za migogoro ya ardhi zimewasilishwa na jamii kutoka maeneo tofauti, huku kesi 1,066 tayari zikiwa zimetatuliwa katika kipindi cha mwaka mmoja. Kwa sasa, Tume inaendelea kuzuru kaunti zote ili kusikiliza na kushughulikia masuala ya ardhi katika ngazi ya jamii.