- 1,034 viewsDuration: 3:03Ubalozi wa Urusi hapa nchini umepinga ripoti ya idara ya ujasusi iliyowahusisha na sakata ya usajili wa wakenya kwenda kupigana katika vita kati ya Urusi na Ukraine. Ubalozi huo kwenye taarifa umesema kuwa ripoti hizo si za kweli na kusema kamwe hawajakuwa wakitoa stakabadhi kwa wakenya kusafiri kuelekea jijini Moscow kwa vita. Haya yamejiri huku familia za wakenya walioelekea Urusi zikitaka bunge na serikali kuingilia kati kuwarejesha jamaa zao nchini