- 4,649 viewsDuration: 3:34Mwenyekiti wa chama cha ODM Gladys Wanga ametangaza kwamba chama hicho kinataka kipewe asilimia nusu ya utawala wa serikali kabla ya kufanya muungano na chama cha UDA kufikia uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027. Na huku Wanga na viongozi wengine wakipiga mirindimo ya muungano, naibu kinara wa chama hicho Godfrey Osotsi amepinga muungano wowote na chama cha Rais William Ruto akisisitiza kwamba ni sharti chama hicho kiwe na mgombea urais debeni.