Viongozi wanashinikiza kuongezwa kwa rasilimali ili kuhakikisha mpito wa asilimia mia moja kutoka shule za msingi hadi sekondari.
Viongozi hao wamesema kuwa bado kuna changamoto zinazokwamisha utekelezaji wa sera hiyo, akisisitiza umuhimu wa ufadhili wa kutosha kwa shule za umma. Aidha wameitaka serikali kushughulikia malalamishi ya walimu, yakiwemo masuala ya bima ya afya ya SHA, pamoja na malipo ya kusahihisha mitihani na maslahi mengine.Viongozi hao walizungumza katika Shule ya Msingi ya Enoomatasian huko kajiado kaskazini wakati wa uzinduzi wa madarasa.