Ukeketaji wakithiri Samburu

  • | Citizen TV
    103 views

    Swala la tohara ya mtoto wa kike katika jamii ya wafugaji, limesalia kuwa kero katika jamii ya wasamburu. Ongezeko ya visa hivyo vikiripotiwa wakati wa likizo,hali ambayo imewakera wakereketwa ambao wameelezea wasiwasi wao na kuitaka serikali kuwachukulia hatua wanaoendeleza mila hiyo iliyoharamishwa . Takwimu zinaashiria kuwa kaunti hiyo imerekodi asilimia 75 ya visa hivyo kama anavyoarifu mwanahabari wetu Bonface Barasa.