Ulaghai wa malipo ya SHA | Mabilioni ya pesa za SHA kwenye hatari ya kufujwa

  • | Citizen TV
    66 views

    Mabilioni ya pesa yaliyowekezwa kwenye mfumo mpya wa usimamizi wa huduma za afya, sasa yako hatarini huku utata mpya ukizonga bima ya matibabu ya SHA. Wizara ya afya inasema kuwa imekataa kulipa madai ya shilingi bilioni10.6 zinazodaiwa na vituo vya afya. Haya ni huku mtafaruku ukiibuka mitandaoni kuhusiana na madai kuwa fedha za hazina ya bima ya afya ya jamii zinatolewa kwa vituo hewa vya matibabu.