- 107 viewsUlinzi Stars wamenusurika kushuka daraja kutoka Ligi Kuu ya Kenya baada ya ushindi wa 2-0 nyumbani dhidi ya Tusker FC katika Ulinzi Complex. Kariobangi Sharks kwa upande mwingine walitoka sare ya 1-1 na Police FC na watalazimika kwenda kwenye mchujo ili kunusurika au kushushwa daraja ikiwa sheria mpya zitatekelezwa. Mabingwa Gor Mahia walitoka sare tasa dhidi ya Mara Sugar huko Homa Bay.