- 784 viewsDuration: 2:29Zoezi la Usajili wa Wapiga Kura linakamilika rasmi hapo kesho huku Tume ya Uchaguzi (IEBC) ikifanya kila juhudi kufikia azma yake ya kuwaandikisha wapiga kura wapya milioni 2.5. Tume hiyo ikisema kuwa hadi sasa watu milioni 1.8 wamejisajili huku kaunti za Nairobi na Kiambu zikiongoza kwa idadi ya juu ya wapiga kura wapya. Kaunti za Lamu, Isiolo na Mandera zimeandikisha idadi ya chini ya waliojisajili.