- 341 viewsDuration: 1:41Baadhi ya wakazi wa kaunti ya Busia wameitaka IEBC kuwajibika na kuhakikisha kuwa uchaguzi mkuu ujao ni wa haki na huru. Wakizungumza katika kaunti ya Busia, wakazi hao wanasema kuwa wako tayari kupiga kura mwaka ujao kwa asilimia 100 wakiwataka maafisa hao kutekeleza majukumu yao kwa uwazi. Wamesikitika kuwa licha ya idadi ya wapiga kura kuongezeka, baadhi yao hukosa kupiga kura kwa kuhofia kuwa kura hitaibwa.