- 98 viewsDuration: 2:06Wanafunzi kutoka kaunti ya Garissa wamehimizwa kusomea kozi zitakazowawezesha kupata ujuzi wa kujiajiri wenyewe. Kwenye kongamano la kushauri wanafunzi kuhusu nafasi za kupata ajira kwenye mataifa ya ugaibuni katika chuo kikuu cha Garissa, watalamu wa nyanja mbali mbali za elimu walielezea umuhimu wa kuwa na ujuzi maalum utakaowapa nafasi hizo. Aidha serikali imetakiwa kuharakisha muda wa kupata pasipoti nchini ili kupunguza mahangaiko kwa wanaotafuta ajira katika mataifa ya nje.