- 312 viewsDuration: 1:22Muungano wa Maaskofu katika kaunti ya Bungoma wamekashfu wanasiasa ambao wanaendeleza siasa za kuchafuliana majina na badala yake kuwataka kuuza sera zao kwa wananchi kwa njia ya Uadilifu. Wakihutubia wanahabari mjini Bungoma katika Kanisa la Ack, wakiongozwa na Askofu George Mechumo viongozi hao wa kidini wanasema kuwa ni masikitikio makubwa kuona viongozi wakirushiana cheche za matusi hadharani wakati ambapo mwananchi wana matarajio ya miradi ya maendeleo kutoka kwao.